Sunday, September 14, 2014

PINDA "KUTAJWA URAIS NI VYEMA"


Waziri Mkuu Mizengo Pinda. PICHA|MAKTABA 


Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema kuwa siyo jambo baya kwake kutajwa kutaka kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao 2015 na kwamba kujitokeza pia ni jambo jema.

 Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili nyumbani kwake mjini Dodoma juzi, ambapo alizungumzia mambo mbalimbali, Pinda alisema kuwa jambo la msingi kwa wote wenye nia ya kuwania nafasi hiyo ya juu ya uongozi nchini ni kutambua kuwa urais ni dhamana kutoka kwa wananchi na haupatikani kwa uamuzi wa anayegombea, bali taratibu za vyama na wananchi watakaopiga kura.

 Pinda maarufu kama Mtoto wa Mkulima alisema pia kwamba ni muhimu kwa watu wanaotaka kuwania urais wasikiuke misingi ya haki kwa kuingilia mchakato na kuwadhoofisha watu wenye mamlaka ya kuchagua mgombea urais, bali waachwe ili wafanye uamuzi wa haki kwa manufaa ya taifa, huku akisisitiza kufuatwa kwa taratibu za Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Kujitokeza ni jambo jema, kutajwatajwa nako pia ni jambo jema tu kwa maoni yangu. Ninachoweza kusema kikubwa, wote wanaotaka kwenda kwenye hiyo nafasi, rai yangu kubwa ni moja tu, watambue wanachotaka kwenda kufanya ni dhamana. Ni nafasi kubwa, lakini ni dhamana tu unapewa kwa niaba ya Watanzania wengine wote.Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAAFISA 10 WAKATAA KURUDI NCHINI LIBERIA

Rais Sirleaf Johnson wa Liberia
Rais wa Liberia Sirleaf Johnson amewafuta kazi maafisa kumi wa serikali kwa kukataa kurudi nchini humo wakati ambapo taifa hilo linakabiliana na maambukizi hatari ya ugonjwa wa Ebola.
Maafisa hao waliagizwa kurudi nchini humo mwezi mmoja uliopita.
Rais Sirleaf amewashtumu kwa kutojali janga linalowakumba raia wa taifa hilo.
Bi Sirleaf ameripotiwa kuomba msaada zaidi kwa serikali ya rais Obama ili kukabiliana na virusi hivyo.
Ameitaka Marekani kujenga kituo kimoja cha kuwatibu wagonjwa wa Ebola katika mji mkuu wa Monrovia.
Virusi hivyo vimewaua zaidi ya watu 2,400 Magharibi mwa Afrika tangu mwezi Machi ,nusu ya raia hao wakitoka nchini Liberia. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MATEKA MWINGINE AKATWANKICHWA NA IS

David Haines
Serikali ya Uingereza imesema kuwa inachukua hatua za dharura ili kubaini ukweli wa kanda ya video inayoonyesha mateka wa Uingereza David Haines aliyetekwa nyara na kundi la himaya ya kiislamu akikatwa kichwa.
Mfanyikazi huyo wa misaada aliyekamatwa nchini Syria mnamo mwezi Machi mwaka jana ameonyeshwa akipiga magoti katika jangwa, kando yake akiwa ni mtu aliyeficha uso wake ambaye amebeba kisu.
Atakuwa mateka wa tatu wa magharibi kukatwa kichwa katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita.
katika kanda hiyo ya Video mtu aliyeshika kisu anaonekana akishtumu mataifa yanayounga mkono Marekani,naye Haines ambaye anaonekana kuwa chini ya shinikizo anaonekana akimlaumu waziri mkuu nchini Uingereza David Cameron kwa hatma yake.
Mwisho wa kanda hiyo mateka wa pili wa Uingereza anaonyeshwa na kutishiwa.
David Cameron
Wakati huohuo Waziri mkuu nchini Uingereza David Cameron ameshtumu kukatwa kichwa kwa David Haines kama kitendo cha kishetani.
Amesema kuwa wauaji watakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria ata iwapo itachukua mda mrefu.
Katika taarifa yake rais Obama pia ameshtumu mauaji ya kikatili ya David Haines.
Amesema Marekani inaomboleza na Uingereza kifo cha mateka huyo na kungezea kuwa itashirikiana na muungano mkubwa wa kimataifa ili kuwakamata washukiwa mbali na kuharibu tishio hilo kwa ulimwengu.
Wanahabari wawili Steven Sotlof na james Foley waliuawa na wapiganaji hao mwezi uliopita. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, September 12, 2014

OSCAR HATIANI KWA KUMUUA MPENZI WAKE BILA KUKUSUDIA

Mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius, amepatikana na hatia ya kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp kwa bahati mbaya
Akitoa uamuzi wake jaji Thokozile Masipaal alisema kuwa mwanariadha huyo alimuua Reeva kwa bahati mbaya alipofyatua risasi kupitia kwa mlango wake wa choo akiw akatika hali ua mshtuko akidhani kuwa jambazo alikuwa amevamia nyumba yake.
Alisema kuwa upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha kuwa Pistorius alinuia kumuua Steenkamp nw akutekeleza mauaji hayo kwa kusudi.
Pia alipatikana na hatia ya kosa la kutumia silaha yake visivyo alipokwenda mgahawani

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC SWAHILI

CHEYO AWAVAA UKAWA BUNGENI, ADAI HAWAKUKUBALIANA NA RAIS KULIVUNJA BUNGE...!!!




Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, John Cheyo akichangia mjadala kuhusu sura mbalimbali za kwenye Rasimu ya Katiba, mjini Dodoma jana.


Mwenyekiti wa Taasisi ya Demokrasia Tanzania (TCD), John Cheyo amewavaa viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), akieleza kuwa walichokubaliana katika kikao chao na Rais Jakaya Kikwete ni kwamba Bunge liahirishwe Oktoba 4 na si kama wanavyodai wakiwa nje.

Akizungumza bungeni mjini Dodoma jana, Cheyo alisema hakuna makubaliano ya kutaka Bunge lisitishwe kabla ya kukamilisha kazi zake Oktoba 4, ikiwamo kutoa Katiba itakayopendekezwa kwa wananchi.

“Mojawapo tulilokubaliana ni Bunge hili lipate Katiba itayopendekezwa kwa wananchi,” alisema Cheyo huku akipigiwa makofi na kelele kutoka kwa baadhi ya wajumbe.

“Pia tulikubaliana kwa hali halisi ya muda tulionao, haiwezekani mchakato mzima ukamalizika na maana ya kumalizika mchakato ni kura ya maoni ya wananchi na ndiyo wenye Katiba.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MTOTO ALIYEZAMIA NDEGE NA KUTUA ZANZIBAR UTATA MTUPU



Uwanja wa ndege wa Zanzibar  


Polisi Zanzibar wameanza uchunguzi kubaini mazingira ya safari tata ya mtoto Karine Godfrey aliyesafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar kwa ndege bila tiketi wala kugundulika.

Mtoto huyo, Karine au Jenipher Godfrey anayesoma darasa la tatu katika Shule ya Msingi Jitihada, Dar es Salaam alionekana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Septemba Mosi saa 11.30 jioni, akieleza kuwa aliingia Zanzibar kwa ndege ambayo hata hivyo, haikufahamika mara moja ni ya shirika gani.

Alikutwa uwanjani hapo akijiandaa kuondoka kwenda mahali asipopajua.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis alisema mbali ya kushangazwa na mazingira ya safari ya mtoto huyo, polisi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar wanalifanyia kazi suala hilo.

“Ni jambo la kushangaza. Tunajiuliza, huyu mtoto alifikaje katika ndege bila ya kuwa na tiketi wala taarifa zozote kuelezea safari yake na je, huko Dar es Salaam aliondokaje hadi kuingia katika ndege bila ya hivyo vitu, sielewi ilikuwaje. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 12, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.
.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SITTA ASHUKIWA KAMA MWEWE...!!!



Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta akizungumza bungeni. Picha na Maktaba 


Mpango wa Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta wa kutaka ya wajumbe wake walioko nje ya nchi kupiga kura kupitisha Katiba inayopendekezwa, umepingwa na wasomi, ukielezwa ni kinyume na kanuni za Bunge na sheria za nchi.

Wasomi hao, wanaharakati na wanasiasa wamesema Tanzania haina utaratibu wa raia wake kupiga kura wakiwa nje ya nchi na kwamba hiyo ni mbinu ya kufanya udanganyifu.

Juzi, Sitta alisema wajumbe wa Bunge hilo watakaokuwa nje ya nchi kwa sababu zozote, ikiwamo ya matibabu na Hijja, watapiga kura hukohuko mara upigaji kura utakapoanza Septemba 26, mwaka huu na kuwataka wajumbe hao kuacha mawasiliano yao watakapokuwa nje na kwamba uongozi wa Bunge umeanza kufanya mawasiliano na balozi mbalimbali za Tanzania, ili wawepo watumishi wake watakaokula kiapo cha kisheria kusimamia kazi hiyo.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana alisema suala la Watanzania kupiga kura wakiwa nje ya nchi halimo kwenye kanuni zinazoongoza Bunge hilo na ni vizuri utaratibu huo ukaachwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

AAMRISHWA KUACHA KUSAMBAZA HIV...!!!

Takriban watu 50,000 nchini Marekani huambukizwa virusi vya HIV kila mwaka
Jaji nchini Marekani amemuamrisha mwanamume mmoja mwathiriwa wa virusi vya HIV kukoma kusambaza virusi hivyo na badala yake kupata matibabu.
Inaarifiwa mwanamume huyo amewaambukiza watu 8 virusi kwa kukusudia katika kipindi cha miaka minne
Mwanamume huyo, aliyetambuliwa tu kwa herufi...'AO' katika stakabadhi zake, ametakiwa na mahakama kupata ushauri nasaha ili aweze kuwakinga wapenzi wake katika siku za usoni.
Maafisa wanasisitiza kwamba sio lengo lao kuufanya uhusiano wa kimapeni kuwa uhalifu bali wanataka zaidi kulinda umma.
Mwanamume huyo huenda akatozwa faini au kufungwa jela ikiwa hatafuata sheria kama alivyotakiwa.
Takriban watu 50,000 nchini Marekani huambukizwa virusi vya HIV kila mwaka , kulingana na shirika la kupambana na maambukizi (CDC).
Asilimia 16% ya watu milioni 1.1 wanaishi na virusi vya HIV bila ya kujua kwamba wameambukizwa.
Mwanamume huyo, alipatikana na virusi vya HIV mwaka 2008 na kuanza kusambaza kwa watu wengine na hadi sasa watu 8 wamethiriwa baada ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi naye.
Alisambaza virusi hivyo licha ya kupokea ushauri nasaha ikiwemo kutumia kinga kila wakati anapojihusisha na tendo la ndoa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...