Tuesday, September 17, 2013

WATUHUMIWA WA MAUAJI YA BILIONEA ERASTO MSUYA WAKUTWA KWA SANGOMA

Jeshi la polisi mkoa wa kilimanjaro linawashikilia watu wanne zaidi wakidaiwa kuhusika na mauaji ya mfanyabiashara bilionea wa madini ya tanzanite Arusha Erasto Msuya 43 wawili kati yao walikutwa kwa mganga wa kienyeji (sangoma) wakifanyiwa zindiko ili wasikamatwe na vyombo vya dola.

Pia jeshi limenikiwa kunasa bunduki aina ya SMG yenye namba za usajili KJ10520,inayoaminika kutumika katika mauaji hayo.Msuya aliuawa kwa kupingwa risasi zaidi ya 10 kifuani Augost 7mwaka huu,katika eneo la mijohoroni wilayani Hai.

Akizungumza na waandishi wa habari jana,kamanda wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Robert Boaz aliwataja watuhumiwa kuwa ni Sadiki Jabiri 32 mkazi wa Dar es Salaam na Lang'angata wilayani Hai .

MWALIMU AKAMATWA AKIWAFANYIA WANAFUNZI MTIHANI WA DARASA LA SABA IRINGA

Jeshi la  polisi  mkoani Iringa  linamshikilia mwalimu wa  shule ya msingi Makungu wilaya ya  Mufindi Bw Edwin Ambukile kwa  tuhuma  za  kuwasaidia majibu wanafunzi wa  darasa la  saba katika mtihani  wa Taifa  wa kuhitimu elimu ya msingi.
Kamanda  wa polisi mkoa  wa Iringa Bw Ramadhan Mungi amesema  kuwa tukio  hilo limetokea  Septemba 15 mwaka  huu  .
Alisema kuwa mwalimu  huyo ambae ni mwalimu wa masomo ya Sayansi katika  shule  hiyo pia alikuwa ni mwalimu wa masomo ya ziada ( katika  shule  hiyo na  sababu ya  kuwasaidia  wanafunzi majibu ni kutaka  kupata umaarufu kwa wanafunzi  watano aliokuwa akiwafundisha masomo ya  ziada aliopata  kuwaahidi kuwa watafaulu mtihani  huo.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE SEPTEMBA 17, 2013

DSC 0094 87348
DSC 0095 5e40c

KINANA AMPONZA BALOZI WA CHINA... CHADEMA KUMSHITAKI KWENYE MAHAKAMA YA KIMATAIFA

http://3.bp.blogspot.com/-tB-YS2RGEHk/UjfrTKmUq2I/AAAAAAAAl3k/wO2eYdRF-0M/s1600/1.png
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kitamshitaki Balozi wa China nchini, Lu Younqing Umoja wa Mataifa (UN) kwa kukiuka Mkataba wa Vienna (Vienna Convention) wa mwaka 1964 ambao unaeleza uhusiano wa kibalozi kati ya nchi na nchi.


Aidha, kimesema kitaiandikia barua Serikali ya China ili kutaka ufafanuzi kama imemtuma Balozi wake kufanya kazi ya uenezi siasa kwenye vyama.


Tukio la Balozi huyo kuhudhuria mkutano wa hadhara wa CCM lilitokea Septemba tisa mwaka huu kwenye mkutano wa chama hicho uliofanyika Wilaya ya Kishapu Shinyanga, ambapo Katibu Mkuu wake, Abdulrahman Kinana alimtambushisha balozi huyo huku akiwa amevaa sare za chama hicho.

WAMALAWI WAMIMINIKA KATIKA OFISI ZA UHAMIAJI JIJINI DAR KWAAJILI YA KUJIORODHESHA UHALALI WA KUISHI TANZANIA

Raia wa Malawi wakiwa katika foleni ya kuingia kujiandikisha katika Idara ya Uhamiaji, Mkoa wa Dar es Salaam jana kuhusu zoezi linaloendelea la kuwatambua wahamiaji haramu jijini Dar es Salaam. Mamia ya wakazi hao walimiminia katika ofisi hizo leo kujiorodhesha ikiwa ni agizo la Rais Jakaya Kikwete.
Akina mama na watoto wakisubiri kujiorodhesha.
Ofisa wa Uhamiaji akiwaelekeza jambo Raia wa Malawi. Credits: Father Kidevu Blog

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...