Shilingi
bilioni 67.7 zimelipwa na Serikali kwa vyama vya siasa katika kipindi
cha miaka 4, 2009/2010 mpaka 2012/2013. Fedha hizi hazijakaguliwa kwa
mujibu wa Sheria.
Mahesabu
ya Vyama vya siasa nchini yanapaswa kukaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Mahesabu ya Serikali kwa mujibu wa Sheria tangu mwaka 2009.
Tangu mwaka huo Kamati ya PAC haijawahi kuona Taarifa ya CAG kuhusu
ukaguzi wa vyama vya siasa.
Kamati
imemwita Msajili wa vyama ili kufafanua ni kwa nini Vyama vya Siasa
nchini havifuati sheria (vifungu vya sheria vimeambatanishwa hapa
chini). Uvunjifu huu wa Sheria ni wa makusudi au wa kutokujua? Sheria
inataka Mahesabu ya vyama yatangazwe kwa uwazi, tena kwa Government
Notice. Umewahi kuona?



Vijana
wa Halaiki wakitoa burudani kwa kuimba nyimbo mbalimbali
zinazohamasisha umoja wa taifa leo wakati wa kilele cha mbio za mwenge
wa uhuru katika viwanja vya Samora mjini Iringa.
Wakimbiza Mwenge wa Uhuru 2013 wakiingia katika viwanja vya CCM Samora mkoani Iringa leo.
Kiongozi wa mbi za Mwenge wa Uhuru 2013 Bw. Juma Ali Simai akisoma
risala ya ujumbe wa wananchi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mh. Jakaya Kikwete leo mjini Iringa.
Rais Jakaya Kikwete (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wakimbiza mwenge wa Uhuru 2013 leo mjini Iringa.
Rais Jakaya Kikwete na mama Salma Kikwete (wa tatu kutoka kushoto)
wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wizara ya Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo wakiongozwa na Waziri wa Wizara hiyo Dkt. Fenella
Mukangara (wa nne kutoka kushoto)
Wananchi
wa mkoa wa Iringa na vijana wa halaiki wakifuatilia matukio mbalimbali
wakati wa Kilele cha mbio za Mwenge leo mkoani Iringa.