Wednesday, November 19, 2014

WAPINZANI WAMSULUBU MWAKYEMBE BUNGENI



Dk Harrison Mwakyembe
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, jana ilimsulubu Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe ikieleza kuwa wizara yake iliingia mkataba wa mradi wa treni za kisasa kutoka Stesheni ya Dar es Salaam hadi Pugu kupitia Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) bila kufuata taratibu.
Kambi hiyo ililieleza Bunge kuwa mkataba huo ulisainiwa baina ya mmiliki wa Kampuni ya M/s Shumoja, Robert Shumake na Shirika la Reli Tanzania huku Waziri Mwakyembe akishuhudia.
Msemaji Mkuu wa kambi hiyo, Ofisi ya Waziri Mkuu,  Uwekezaji na Uwezeshaji, Pauline Gekul alitoa madai hayo wakati akiwasilisha maoni ya kambi hiyo kuhusu muswada wa marekebisho ya Sheria ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP). Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

NABII: "URAIS 2015 BALAA!... JK ASINGEWAHI KUPASULIWA, NCHI INGECHAFUKA"




NABII wa Kanisa la The Revelation lililopo Buza Kipera jijini Dar, Yaspi Bendera amesema uchaguzi mkuu ujao utakuwa balaa kubwa kufuatia maono anayoyaona wakati akishiriki ibada katika nyakati mbalimbali, Risasi Jumatano linakupa mkanda kamili.

Nbii wa Kanisa la The Revelation lililopo Buza Kipera jijini Dar, Yaspi Bendera.

Akizungumza wakati wa ibada kanisani kwake na baadaye na waandishi wetu Novemba 16 mwaka huu, Nabii Yaspi alisema kuna mgongano mkubwa miongoni mwa watu wanaotajwa kugombea urais, ili kumrithi rais Jakaya Kikwete ambaye alimwelezea kama kiongozi anayemuona kiroho kila mara.


“Nilimuona katika maono yangu kama mtu aliye kwenye majaribu makubwa kiroho, nikaandaa maombi hapa kanisani na tukamuombea kwa muda wa nusu saa na tunashukuru Mungu hali yake inaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji wa tezi dume nchini Marekani. Bado namuona akiwa na maumivu kuanzia sehemu za kiuno, uti wa mgongo na shingoni mwake.

Mhe. Edward Lowasa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

UJERUMANI YAIUA HISPANIA 1-0

Mario Gotze, who scored Germany's winning goal at the World Cup final, is put under pressure by Cesar Azpiliciueta and Sergio Busquets 
Mario Gotze akiwapita Cesar Azpiliciueta wa Sergio Busquets wa Hispania katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa mjini Vigo. Ujerumani ilishinda 1-0, bao pekee la Toni Kroos dakika ya mwisho.
Gotze is grounded under the challenge of Spain defender Sergio Ramos as the rain beings to fall in Vigo on Tuesday evening
Gotze akienda chini baada ya kukwatuliwa na beki wa Hispania, Sergio Ramos. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Monday, November 3, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 03, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WARIOBA ADHALILISHWA KATIKA MDAHARO WA KATIBA...!!!

Waziri Mkuu mstaafu Joseph Warioba akisaidiwa kutolewa katika vurugu
Katika mazingira ya kutatanisha, jana Jumapili Novemba 02, mwaka huu vurugu zimekatisha mdahalo uliokuwa ukiendelea kujadili mchakato wa katiba mpya ya Tanzania huku baadhi ya watu wakipigwa na kujeruhiwa.
Mdahalo huo uliokuwa ukitangazwa moja kwa moja kupitia redio na televisheni za hapa nchini  ulivurugika kutokana na kundi la vijana wapatao 20 kuanza kumzomea aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, alipokuwa akiwasilisha mada yake.
Vijana hao ambao haijajulikana walitokea wapi au walikuwa na ajenda gani waliinua mabango ya kupinga msimamo wa waliokuwa wakiendesha mdahalo na kusema rasimu ya katiba iliyopendekezwa inakidhi mahitaji yote na kusema hakuna haja ya mdahalo.
Jaji Warioba ambaye ni Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania alifanikiwa kutoka salama nje ya ukumbi ulipokuwa ukifanyika mdahalo huo jijini Dar Es Salaam, lakini wapo watu waliojeruhiwa kutokana na kurushwa viti na vitu vingine. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAANDAMANO ZAIDI YAFANYWA BURKINA FASO



Jeshi la Burkina Faso limefyatua risasi hewani kuwatawanya waandamanaji nje ya kituo cha utangazaji cha taifa katika mji mkuu, Ouagadougou.
Ripoti zinasema kuwa risasi zilifyatuliwa punde baada ya kiongozi wa upinzani, Sara Sereme, kuwasili pamoja na wafuasi wake.
Wanajeshi waliwatawanya maelfu ya waandamanaji waliokusanyika katika medani kuu mjini Ouagadougou.
Vyama vya upinzani vinataka iwekwe serikali ya muda ya raia hadi uchaguzi wa rais utapofanywa.
Mjumbe wa Umoja wa Mataifa mjini humo, Mohamed ibn Chambas, ameonya kuwa Burkina Faso inaweza kuwekewa vikwazo iwapo jeshi litaendelea kuongoza nchi. Asante kwa kutembelea blog hii, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MSIMAMO WA VODACOM PREMIER LEAGUE (VPL) KWA SASA

 
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Tuesday, October 14, 2014

WAZIRI LAZARO NYALANDU AZUNGUMZIA TETESI ZA KUTANUA NA AUNT EZEKIEL NCHINI MAREKANI

  Baada ya vyombo vya habari kuripoti kuhusu Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu(Pichani juu) na msanii wa filamu Aunty Ezekiel kuvinjari nchini Marekani hatimaye waziri huyo 
Aunt Ezekiel
alisema tuhuma hizo zimetengenezwa na kundi la watu ambalo miongoni mwao ni baadhi ya viongozi wa Serikali ambao humchafua kutokana na utendaji kazi wake.

Nyalandu alisema alikwenda Marekani septemba12 kwa ajili ya kufungua tamasha la utamaduni na utalii kupitia soko la wasanii wa Tanzania ambako alikutana na msanii huyo mara moja pamoja na mwingine wa Bongo Fleva Kassim Mganga usiku katika moja ya maeneo nchini humo.

Alikana kutanua na msanii huyo kama baadhi ya nyombo vya habari vilivyoripoti na kusema maneno hayo ni kwa lengo la kumwaribia heshima yake mbele ya jamii. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAMA KANUMBA NA LULU NDANI YA FILAMU MPYA IITWAYO "MAPENZI YA MUNGU"

Hivi karibu Msanii Mahiri na Nguli katika tasnia ya filamu nchini Elizabeth Michael almaarufu kama LULU ataibuka na filamu yake Mpya na yenye kusisimua iitwayo "MAPENZI YA MUNGU" ambapo moja kati ya washiriki katika filamu hiyo ni Bi Flora Mtegoha ambae ni Mama Mzazi wa aliyekuwa Msanii Nguli wa Kiume Hapa Bongo Marehemu Steven Kanumba.

Filamu ya "Mapenzi ya Mungu" ni moja ya filamu ambayo Lulu ameonyesha uwezo wa hali ya na kuthibitisha kuwa ni mmoja kati ya wasanii wa kike hapa Tanzania ambae ana kipaji cha hali ya juu katika kuuvaa uhusika ambapo ana uwezo wa kubadilika badilika kutokana na muongozo anaopewa.

Filamu ya "Mapenzi ya Mungu" itakuwa Sokoni hivi Karibu Kwa Wauzaji wa Filamu kote Nchini.

Filamu hii itasambazwa na Kampuni mahiri ya Proin Promotions Ltd. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAASKOFU KATOLIKI WAUZUNGUMZIA USHOGA


Mkutano wa maaskofu Vatican

Makasisi wanaoshiriki katika mkutano wa maaskofu wanaangazia masuala ya mafunzo ya kanisa katoliki kwa familia ,wametoa mwito kwa kanisa hilo duniani kuwachukulia watu wenye mapenzi ya jinsia moja kwa usawa
Kauli hii inakuja baada ya Maaskofu kuandika ripoti wakati wa mkutano wa synodi ukiendelea huko Vatican na kusema kuwa wapenzi wa jinsia moja wana zawadi na viwango vya kutoa kwenye jumuiya za kikristo hii ikiwa ni ripoti iliyotolewa mapema wiki hii. Ripoti hiyo haitoi changamoto yoyote kwa msimamo wa muda mrefu wa kanisa hilo juu ya kupinga ndoa za jinsia moja,lakini baadhi ya vikundi vya kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja wanachukulia kauli hiyo kuwa ya mafanikio makubwa kwa jamii zao. Na moja ya makundi yenye kushikilia msimamo mkali kikanisa wametupilia mbali ripoti hiyo na kuuita ya kisaliti. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Sunday, October 12, 2014

FILAMU YA YESU ILIYOTAFSIRIWA KWA LUGHA YA KINYAKYUSA



MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 12, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BOKO HARAM LAWAACHIA MATEKA 27

boko haram
Rais wa Cameroon amesema kuwa mateka 27 wakiwemo raia 10 wa Uchina wameachiliwa na kundi la wanamgambo wa Boko Haram.
Raia hao wa China walitekwa nyara mwezi mei wakati kampuni moja ya China ilipovamiwa karibu na mpaka wa Nigeria.
Wengine walioachiliwa ni pamoja na mke wa naibu waziri mkuu nchini Cameroon aliyetekwa nyara mwezi Julai.
Haijulikani iwapo fidia ililipwa.
Boko haramu wameeneza mashambulizi kutoka nchini Nigeria kwenda kaskazini magharibi mwa Cameroon. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MABINGWA WA DUNIA UJERUMANI ‘ YACHAPWA’ KWA MARA YA KWANZA NA POLAND


Poland imeifunga UJerumani kwa mara ya kwanza na kukwea juu ya kilele katika kundi la Nne kuwania nafasi ya kufuzu kwa fainali za Ulaya, Euro, 2016 nchini Ufaransa. Mabingwa wa dunia , Ujerumani ilikuwa na rekodi ya kucheza mara 18 mfululizo bila kupoteza mchezo wowote dhidi ya majirani zao, Poland ambao walipata mabao yote mawili katika kipindi cha pili.
Mshambulizi kinda wa klabu ya Ajax Amsterdam, Arkadiusz Milik, 20 alifunga bao la kuongoza katika dakika ya 51, na dakika mbili kabla ya kumalizika kwa mchezo, Sebastian Mila aliwahakikishia wenyeji ushindi baada ya kufunga bao la pili katika mchezo huo uliopigwa jijini, Warsaw.
Mabingwa hao wa sasa wa dunia, walifungwa mara ya mwisho na Jamhuri ya Czech, Oktoba, 2007 katika michezo ya kufuzu. Ujerumani ilicheza michezo 33 ya kufuzu pasipo kupoteza. Kipa wa Ujerumani, Manuer Neur aliokoa mabao manne ya wazi katika mchezo ambao walishambuliwa sana. Poland iliyokuwa na mshambulizi wa Bayern Munich, Robert Lewandowski ilipiga jumla ya mashuti 19, huku mashuti 12 yakilenga bao.
Kocha wa Ujerumani, Joachim Loew alikwenda Poland huku baaddi ya wachezaji wake muhimu wakikosekana. Ujerumani ilibanwa hasa na walimudu kufanya mashambulizi machache . Walipiga mashuti saba tu ambayo yote yalilenga lango lakini nyota wa mchezo huo, golikipa, Wojciech Szczesny alikuwa imara, kipa huyo wa klabu ya Arsenal aliokoa mara 14. Tomas Mueller, Andre Schurrle na Mario Gotze walishindwa kufunga kwa muda wote waliokuwa uwanjani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

UFARANSA YAICHAPA URENO NA C.RONALDO AKIWEMO

Mshambulizi Karimu Benzema alifunga bao la mapema na akatengeneza lingine kwa kiungo Paul Pogba katika kipindi cha pili na kuisaidia Ufaransa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ureno. RicaRrdo Quaresma alitokea benchi katika kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Luis Nani katika dakika ya 68, alifunga kwa mkwaju wa penalti dakika tisa baada ya kuingia uwanjamni .
Ufaransa ambao ndiyo wenyeji wa fainali zijazo za Ulaya waliifunga Ureno ambayo ilikuwa na mshambulizi wake mahiri na mchezaji bora wa dunia, Cristiano Ronaldo katika mchezo uliofanyika jijini Paris. Ronaldo alipiga mashuti manne katika mchezo huo lakini ni shuti moja tu ambalo lilikuwa na uhai. Timu zote zilicheza mchezo wa kufanana, Ufaransa walipiga mashuti 12 sawa na waliyopiga Ureno, lakini wageni walifanikiwa kupiga mashuti mawili tu ambayo yalimsumbua golikipa, Steven Mandanda.
Eliaguim Mangala, RAfaer Varane, Patrice Evra na Bacary SAgna walianza katika safu ya ulinzi na wanne hao hawakuwekwa majaribuni na kikosi kilichopoteza makali cha Ureno. Ronaldo alitoka uwanjani dakika ya 76 akimpisha Jose Mario alianza sambamba Danny na Nani katika safu ya mbele lakini watatu hao hawakuwa tishio kwa Ufaransa ambao walicheza jumla ya faulo 15 katika mchezo huo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Thursday, October 2, 2014

RAILA ODINGA ATANDIKWA BAKORA HADHARANI...!!!

Mzee Mdzombo anasemekana kutokuwa timamu kiakili
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga amemsamehe mzee aliyempiga bakora katika mkutano wa hadhara wa kisiasa katika jimbo la Kwale Pwani ya Kenya,
Mwanamume huyo, Lengo Mdzombo, anayefanya kibarua katika shamba moja Kwale, alikamatwa Jumanne na kufikishwa mahakamani.
Alishitakiwa kwa kosa la kumshambulia kiongozi huyo pamoja na gavana wa Kwale.
Hali ya taharuki ilitanda katika mkutano wa hadhara Jumatatu wiki hii baada ya Mdzombo kwenda ukumbini na kuanza kumtandika bakora kiongozi wa upinzani Raila Odinga pamoja na wanasiasa wengine.
Raila alikuwa amejiunga na kikundi cha wanawake waliokuwa wanacheza densi ya kitamaduni kuwatumbuiza wageni, pamoja na gavana wa jimbo la Kwale Pwani ya Kenya Salim Mvuruya katika mkutanmo wa kisiasa.
Raila alikuwa ameambatana na viongozi wengine, wakiwemo, Seneta Juma Boy, Hassan Omar, Agnes Zani, James Orengo, Johnstone Muthama na wengineo.
Kiongozi wa upinzani Raila Odinga
Mzee huyo alimpiga bakora Odinga ambaye ni waziri mkuu wa zamani kabla ya kumgeukia gavana wa jimbo hilo na kumchapa mara mbili. Hata hivyo mwanamume huyo alishindwa nguvu na walinzi wa Raila Odinga.
Polisi walithibitisha kuwa walimkamata mwanamume huyo na kumwachilia baada ya kugundua kuwa alikuwa na matatizo ya kiakili.
Haijulikani kwa nini mwanamume huyo alimshambulia Raila ila baadhi wanasema ni kwa sababu alighadhabishwa pale waziri mkuu alipocheza densi na mwanamke aliyesemekana kuwa mke wake ambaye alikuwa katika kikundi cha wanawake waliokuwa wanawatumbuiza wageni waheshimiwa.
Viongozi waliofika walilazimika kusitisha densi hiyo kabla ya mwanamume huyo kushindwa nguvu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

MKUU WA USALAMA MAREKANI JIUZULU

Julia Pierson mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Marekani
Mkuu wa Idara ya Usalama nchini Marekani, aliyekuwa na jukumu la kumlinda Rais Barack Obama, amejiuzulu kufuatia matukio yenye kuhatarisha usalama wa taifa yaliyotokea.
Mkuu huyo wa usalama Julia Pierson alikabidhi barua ya kujiuzulu kwa Waziri wa Usalama wa Ndani, Jumatano.
Siku moja kabla, alikabiliana na maswali ya wajumbe wenye hasira kutoka Baraza la Congress juu ya udhaifu mkubwa wa usalama wa Ikulu ya Marekani
Habari za tukio lingine likimhusisha mtu mwenye silaha kuruhusiwa kuingia katika lifti moja na Bwana Obama kulizidisha kutolewa wito wa kumtaka mkuu wa usalama kujiuzulu.
"Leo, Julia Pierson, mkurugenzi wa usalama wa taifa wa Marekani, amenikabidhi barua ya kujiuzulu, na nimeikubali," Waziri wa Usalama wa Taifa Jeh Johnson aliandika katika taarifa.
"Nampongeza kwa utumishi wake wa miaka 30 katika idara ya usalama na taifa." Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

ARSENAL YAUA 4-1, WELBECK APIGA HAT-TRICK


Mshambuliaji Danny Welbeck akishangilia baada ya kupiga 'hat-trick'.

Alexis Sanchez akiifungia Arsenal bao la tatu dhidi ya Galatasaray.

Welbeck akitupia bao la nne. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger ametimiza miaka 18 akiwa meneja wa klabu hiyo leo.
KLABU ya Arsenal imetoa kichapo cha mabao 4-1 dhidi ya Galatasaray kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya iliyopigwa Uwanja wa Emirates jijini London usiku huu.
Mshambuliaji Danny Welbeck ametupia kambani mabao matatu 'hat-trick' huku bao la nne likiwekwa kimianai na Alexis Sanchez. Katika mtanange huo, kipa wa Arsenal, Wojciech Szczesny alizawadiwa kadi nyekundu baada ya kumfanyia madhambi mshambuliaji wa Galatasaray, Burak Yilmaz.
Ushindi wa leo wa Arsenal umeongeza furaha kwa Meneja wa timu hiyo, Arsene Wenger aliyetimiza miaka 18 akiwa kocha wa klabu hiyo leo.
VIKOSI: 
Arsenal: Szczesny, Chambers, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Flamini, Cazorla, Ozil (Wilshere 77), Sanchez (Ospina 62), Oxlade-Chamberlain (Rosicky 68), Welbeck.
Waliokuwa benchi: Coquelin, Bellerin, Campbell, Podolski.
Galatasaray: Muslera, Chedjou, Felipe Melo, Semih Kaya, Veysel (Bulut 68), Yekta (Altintop 46), Dzemaili, Telles, Sneijder, Pandev (Bruma 68), Burak Yılmaz.
Waliokuwa benchi: Bolat, Balta, Adin, Camdal. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, October 1, 2014

BUNGE LA KATIBA: WALIOPIGA KURA YA HAPANA WATISHIWA MAISHA

Wahudumu  wa Bunge Maalumu la Katiba wakiwa wamebeba masanduku ya kura za wajumbe waliopiga kura za siri kwa Sura ya 11 hadi 19 ya Rasimu ya Katiba inayopendekezwa, mjini Dodoma jana.
Baadhi ya wajumbe wa Bunge la Katiba waliopiga kura za hapana wamelazimika kuondoka Dodoma na kurudi Zanzibar kwa madai ya vitisho walivyopata kutoka kwa wenzao.
Mmoja wa wajumbe hao, Salma Said alisema jana jioni kuwa yeye na wajumbe wenzake wamekataa kuitikia wito wa Mwenyekiti wa Bunge, Samuel Sitta kwenye Kamati ya Mashauriano ili kuhojiwa kuhusu kura hiyo na kutokana na vitisho wanavyopata kutoka kwa wajumbe wenzao wameamua kuondoka Dodoma.
Vitisho hivyo vimeripotiwa muda mfupi baada ya Sitta kuunda Kamati ya Mashauriano ya watu tisa inayoongozwa na Makamu Mwenyekiti, Samia Suluhu Hassan kushughulikia kura hizo zilizopigwa na wajumbe saba zinazoweka njiapanda uwezekano wa kupatikana akidi ya kupitisha Katiba inayopendekezwa.
Wajumbe waliopiga kura za wazi za hapana kwa ibara zote ni Adil Mohamed Adil, Dk Alley Soud Nassor, Fatma Mohamed Hassan, Jamila Ameir Saleh, Salma Hamoud Said, Mwanaidi Othman Twahir na Ali Omary Juma. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MKE WA MUGABE KUSHITAKIWA...!!!

Grace Mugabe kulia
Muungano wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Zimbabwe al maarufu Zinasu, umesema kwamba unawasilisha kesi mahakamani hii leo kutafuta ufafanuzi zaidi wa namna mkewe rais Grace Mugabe alivyopata shahada ya udaktari wa falsafa.
Mwanafunzi mmoja mwanaharakati amesema kuwa ni muhimu kwa taifa hilo kuhifadhi hadhi yake ya elimu.
Baadhi ya watu wamehoji kasi aliyosomea shahada hiyo huku wengine wakidai ni njama za kumuandaa kwa urithi wa kiti cha rais baada ya rais Mugabe.
Gazeti moja linalomilikiwa na serikali , the Herald limechapisha kuwa Bi Grace Mugabe alipata shahada hiyo kwa utafiti wake juu ya mabadiliko ya mfumo wa kijamii na miundo ya familia. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

UCL: MATOKEO YA CHELSEA VS SPORTING LISBON

IMG_7653.PNG
Usiku wa jana watu wawili waliowahi kuwa vipenzi vya nchi ya Ureno – Jose Mourinho na Nemanja Matic walirejea nchini humo katika jiji la Lisbon lakini safari hii wakiwa kama wapinzani.
Huku Mourinho akionekana kuchukua ‘attention’ yote ya vyombo vya habari ndani ya jiji Lisbon, Nemanja Matic alikuwa kasahaulika.
Lakini katika dakika ya 34, mchezaji huyo wa zamani wa Benfica aliifungia goli pekee Chelsea katika mchezo huo.
Matic alifunga goli hilo kwa kichwa baada ya kuachwa bila kukabwa vizuri na mabeki wa Sporting Lisbon.
Mchezaji wa zamani wa Manchester United Luis Nani alikuwa akiitumikia Sporting jana na hakuwa kwenye kiwango kizuri katika kipindi cha kwanza – kipindi cha pili alijitahidi lakini akashindwa kubadili matokeo ya mwisho dhidi ya vijana wa Jose Mourinho.
Takwimu na timu zilizopangwa
Sporting (4-3-3): Patricio 7; Cedric 6, Mauricio 5.5 (Oliveira 63, 6), Sarr 5, J.Silva 5; Mario 6, Carvalho 6, A.Silva 6 (Montero 81); Carrillo 6.5 (Capel 81), Slimani 6, Nani 6.
Subs not used: Marcelo, Jefferson, Martins, Rosell.
Bookings: Carvalho, Mario, Cedric, Mauricio
Manager: Marco Silva
Chelsea (4-2-3-1): Courtois 6; Ivanovic 6, Cahill 6, Terry 6, Luis 6.5; Matic 8, Fabregas 7; Schurrle 5 (Willian 57, 6), Oscar 7.5 (Mikel 71, 6), Hazard 7 (Salah 84); Costa 6.
Subs not used: Cech, Zouma, Azpilicueta, Remy.
Bookings: Ivanovic, Hazard, Luis Filipe, Fabregas
Manager: Jose Mourinho.

Sunday, September 14, 2014

PINDA "KUTAJWA URAIS NI VYEMA"


Waziri Mkuu Mizengo Pinda. PICHA|MAKTABA 


Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema kuwa siyo jambo baya kwake kutajwa kutaka kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao 2015 na kwamba kujitokeza pia ni jambo jema.

 Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili nyumbani kwake mjini Dodoma juzi, ambapo alizungumzia mambo mbalimbali, Pinda alisema kuwa jambo la msingi kwa wote wenye nia ya kuwania nafasi hiyo ya juu ya uongozi nchini ni kutambua kuwa urais ni dhamana kutoka kwa wananchi na haupatikani kwa uamuzi wa anayegombea, bali taratibu za vyama na wananchi watakaopiga kura.

 Pinda maarufu kama Mtoto wa Mkulima alisema pia kwamba ni muhimu kwa watu wanaotaka kuwania urais wasikiuke misingi ya haki kwa kuingilia mchakato na kuwadhoofisha watu wenye mamlaka ya kuchagua mgombea urais, bali waachwe ili wafanye uamuzi wa haki kwa manufaa ya taifa, huku akisisitiza kufuatwa kwa taratibu za Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Kujitokeza ni jambo jema, kutajwatajwa nako pia ni jambo jema tu kwa maoni yangu. Ninachoweza kusema kikubwa, wote wanaotaka kwenda kwenye hiyo nafasi, rai yangu kubwa ni moja tu, watambue wanachotaka kwenda kufanya ni dhamana. Ni nafasi kubwa, lakini ni dhamana tu unapewa kwa niaba ya Watanzania wengine wote.Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAAFISA 10 WAKATAA KURUDI NCHINI LIBERIA

Rais Sirleaf Johnson wa Liberia
Rais wa Liberia Sirleaf Johnson amewafuta kazi maafisa kumi wa serikali kwa kukataa kurudi nchini humo wakati ambapo taifa hilo linakabiliana na maambukizi hatari ya ugonjwa wa Ebola.
Maafisa hao waliagizwa kurudi nchini humo mwezi mmoja uliopita.
Rais Sirleaf amewashtumu kwa kutojali janga linalowakumba raia wa taifa hilo.
Bi Sirleaf ameripotiwa kuomba msaada zaidi kwa serikali ya rais Obama ili kukabiliana na virusi hivyo.
Ameitaka Marekani kujenga kituo kimoja cha kuwatibu wagonjwa wa Ebola katika mji mkuu wa Monrovia.
Virusi hivyo vimewaua zaidi ya watu 2,400 Magharibi mwa Afrika tangu mwezi Machi ,nusu ya raia hao wakitoka nchini Liberia. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MATEKA MWINGINE AKATWANKICHWA NA IS

David Haines
Serikali ya Uingereza imesema kuwa inachukua hatua za dharura ili kubaini ukweli wa kanda ya video inayoonyesha mateka wa Uingereza David Haines aliyetekwa nyara na kundi la himaya ya kiislamu akikatwa kichwa.
Mfanyikazi huyo wa misaada aliyekamatwa nchini Syria mnamo mwezi Machi mwaka jana ameonyeshwa akipiga magoti katika jangwa, kando yake akiwa ni mtu aliyeficha uso wake ambaye amebeba kisu.
Atakuwa mateka wa tatu wa magharibi kukatwa kichwa katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita.
katika kanda hiyo ya Video mtu aliyeshika kisu anaonekana akishtumu mataifa yanayounga mkono Marekani,naye Haines ambaye anaonekana kuwa chini ya shinikizo anaonekana akimlaumu waziri mkuu nchini Uingereza David Cameron kwa hatma yake.
Mwisho wa kanda hiyo mateka wa pili wa Uingereza anaonyeshwa na kutishiwa.
David Cameron
Wakati huohuo Waziri mkuu nchini Uingereza David Cameron ameshtumu kukatwa kichwa kwa David Haines kama kitendo cha kishetani.
Amesema kuwa wauaji watakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria ata iwapo itachukua mda mrefu.
Katika taarifa yake rais Obama pia ameshtumu mauaji ya kikatili ya David Haines.
Amesema Marekani inaomboleza na Uingereza kifo cha mateka huyo na kungezea kuwa itashirikiana na muungano mkubwa wa kimataifa ili kuwakamata washukiwa mbali na kuharibu tishio hilo kwa ulimwengu.
Wanahabari wawili Steven Sotlof na james Foley waliuawa na wapiganaji hao mwezi uliopita. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, September 12, 2014

OSCAR HATIANI KWA KUMUUA MPENZI WAKE BILA KUKUSUDIA

Mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius, amepatikana na hatia ya kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp kwa bahati mbaya
Akitoa uamuzi wake jaji Thokozile Masipaal alisema kuwa mwanariadha huyo alimuua Reeva kwa bahati mbaya alipofyatua risasi kupitia kwa mlango wake wa choo akiw akatika hali ua mshtuko akidhani kuwa jambazo alikuwa amevamia nyumba yake.
Alisema kuwa upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha kuwa Pistorius alinuia kumuua Steenkamp nw akutekeleza mauaji hayo kwa kusudi.
Pia alipatikana na hatia ya kosa la kutumia silaha yake visivyo alipokwenda mgahawani

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC SWAHILI

CHEYO AWAVAA UKAWA BUNGENI, ADAI HAWAKUKUBALIANA NA RAIS KULIVUNJA BUNGE...!!!




Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, John Cheyo akichangia mjadala kuhusu sura mbalimbali za kwenye Rasimu ya Katiba, mjini Dodoma jana.


Mwenyekiti wa Taasisi ya Demokrasia Tanzania (TCD), John Cheyo amewavaa viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), akieleza kuwa walichokubaliana katika kikao chao na Rais Jakaya Kikwete ni kwamba Bunge liahirishwe Oktoba 4 na si kama wanavyodai wakiwa nje.

Akizungumza bungeni mjini Dodoma jana, Cheyo alisema hakuna makubaliano ya kutaka Bunge lisitishwe kabla ya kukamilisha kazi zake Oktoba 4, ikiwamo kutoa Katiba itakayopendekezwa kwa wananchi.

“Mojawapo tulilokubaliana ni Bunge hili lipate Katiba itayopendekezwa kwa wananchi,” alisema Cheyo huku akipigiwa makofi na kelele kutoka kwa baadhi ya wajumbe.

“Pia tulikubaliana kwa hali halisi ya muda tulionao, haiwezekani mchakato mzima ukamalizika na maana ya kumalizika mchakato ni kura ya maoni ya wananchi na ndiyo wenye Katiba.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MTOTO ALIYEZAMIA NDEGE NA KUTUA ZANZIBAR UTATA MTUPU



Uwanja wa ndege wa Zanzibar  


Polisi Zanzibar wameanza uchunguzi kubaini mazingira ya safari tata ya mtoto Karine Godfrey aliyesafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar kwa ndege bila tiketi wala kugundulika.

Mtoto huyo, Karine au Jenipher Godfrey anayesoma darasa la tatu katika Shule ya Msingi Jitihada, Dar es Salaam alionekana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Septemba Mosi saa 11.30 jioni, akieleza kuwa aliingia Zanzibar kwa ndege ambayo hata hivyo, haikufahamika mara moja ni ya shirika gani.

Alikutwa uwanjani hapo akijiandaa kuondoka kwenda mahali asipopajua.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis alisema mbali ya kushangazwa na mazingira ya safari ya mtoto huyo, polisi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar wanalifanyia kazi suala hilo.

“Ni jambo la kushangaza. Tunajiuliza, huyu mtoto alifikaje katika ndege bila ya kuwa na tiketi wala taarifa zozote kuelezea safari yake na je, huko Dar es Salaam aliondokaje hadi kuingia katika ndege bila ya hivyo vitu, sielewi ilikuwaje. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...