Sunday, April 19, 2015

MKUU WA KANISA LA ANGLIKANA AZURU MISRI

Justin Welby Katikati
Askofu mkuu wa Cantebury ,Justin Welby anawatembelea viongozi wa kisiasa pamoja na wale wa kidini nchini Misri ili kuzungumzia kuhusu mashambulizi ya hivi karibuni dhidi ya wakristo katika eneo la mashariki ya kati.

Askofu huyo ambaye ndio kiongozi wa Kanisa la Anglikana anatarajiwa kukutana na rais wa Misri Abdul Fattah al Sisi.

Pia atatoa rambirambi zake kwa wakristo wa kanisa la Coptic ambao walitekwanyara na kuuawa na wanamgambo wa Islamic State nchini Libya mnamo mwezi wa Februari.
Askofu huyo amesema kuwa utekajinyara wa wakristo katika eneo hilo ni m'baya zaidi kwa karne kadhaa.

Pia atakutana na Imam mkuu wa chuo cha al-Azhar ambacho ndio taasisi kuu nchini Misri na inaheshimiwa na waislamu wa Sunni kama taasisi kubwa zaidi ya mafunzo ya kiislamu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

UKRAINE: WAASI WADAIWA KUKIUKA MKATABA

wanajeshi wa Ukraine wakijiandaa kuwashambulia waasi
Serikali ya Ukraine inasema kuwa waasi wanaungwa mkono na Urusi wamekiuka pakubwa muafaka wa amani mara 20 zaidi.

Muafaka huo uliafikiwa kusitisha vita katika mji wa Donetsk ulioko mashariki mwa Ukraine.
Duru kutoka kusini mashariki mwa Ukraine, zinasema kuwa kumeshuhudiwa mapigano mapya kati ya wanajeshi waaminifu kwa serikali na waasi wanaoungwa mkono na Urusi.

Mapigano yamechacha katika kijiji cha Shyrokyne - kilichoko katika mji wa bandarini wa Mariupol. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TAZAMA PICHA ZA MNYAMA ALIVYOCHINJWA NA MBEYA CITY JANA

IMG_9679
WEKUNDU wa Msimbazi Simba wamefungwa magoli 2-0 na Mbeya City katika mechi ya ligi kuu soka Tanzania bara iliyochezwa uwanja wa Sokoine Mbeya jioni ya jana.
Kwa matokeo hayo Simba imeendelea kubaki nafasi ya tatu kwa pointi zake 35 baada ya kucheza mechi 22 nyuma ya mabingwa Azam fc wenye pointi 42  baada ya kushinda mechi yao jana mabao 2-1 dhidi ya Kagera. Azam nao wamecheza mechi 22. 
Vinara bado wanabaki kuwa Yanga kwa pointi 46 baada ya kucheza mechi 21.
Magoli ya Mbeya City yalifungwa na Paul Nonga dakika ya 45 kipindi cha kwanza akipokea pasi kutoka kwa Deus Kaseke. City walifunga goli la pili dakika ya 69 kupitia kwa Peter Mwalyanzi.
 Simba ilipata pigo dakika ya 23 baada ya beki wake na nahodha, Hassan Isihaka kuumia na nafasi yake ikachukuliwa na Mganda Joseph Owino
 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

BALOTELLI NDIYE ALIYEBAGULIWA ZAIDI EPL

Mario Balotelli
Mario Balotelli ndiye mchezaji aliyebaguliwa sana katika ligi ya Uingereza ,huku mchezaji huyo akipokea zaidi ya ujumbe 8000 ,asilimia 50 zikiwa ni za kibaguzi.

Takwimu hizo za kushtua zimeripotiwa na Kick it Out ,ambao walibaini kwamba raia huyo wa Itali alilengwa sana katika mitandao ya Twitter huku mshambuliaji wa Arsenal Danny Welbeck akipokea ujumbe 1700 asilimia hamsini zikiwa za kibaguzi.

Mshambuliaji mwenza wa Balotelli katika kilabu ya Liverpool Daniel Sturridge pia alionekana kulengwa katika mitandao ya kijamii baada ya kupokea ujumbe wa 1600 asilimia 60 ikiwa ni ujumbe wenye mwelekeo wa kijinsia.

Utafiti huo pia umebaini kwamba kilabu ya Chelsea ndio kilabu iliobaguliwa zaidi kwa ujumbe 20,000 huku liverpool ikiwa ya pili na ujumbe 19,000 Arsenal ikiwa ya tatu kwa ujumbe 12,000 huku Manchester City na Manchester United zikipokea ujumbe 11,000. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...