Sunday, September 14, 2014

MAAFISA 10 WAKATAA KURUDI NCHINI LIBERIA

Rais Sirleaf Johnson wa Liberia
Rais wa Liberia Sirleaf Johnson amewafuta kazi maafisa kumi wa serikali kwa kukataa kurudi nchini humo wakati ambapo taifa hilo linakabiliana na maambukizi hatari ya ugonjwa wa Ebola.
Maafisa hao waliagizwa kurudi nchini humo mwezi mmoja uliopita.
Rais Sirleaf amewashtumu kwa kutojali janga linalowakumba raia wa taifa hilo.
Bi Sirleaf ameripotiwa kuomba msaada zaidi kwa serikali ya rais Obama ili kukabiliana na virusi hivyo.
Ameitaka Marekani kujenga kituo kimoja cha kuwatibu wagonjwa wa Ebola katika mji mkuu wa Monrovia.
Virusi hivyo vimewaua zaidi ya watu 2,400 Magharibi mwa Afrika tangu mwezi Machi ,nusu ya raia hao wakitoka nchini Liberia. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...