
Serikali za Rwanda, Uganda, Kenya na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, zimefunguliwa kesi katika Mahakama ya Afrika ya Mashariki, zikidaiwa kukiuka mkataba wa kuanzishwa kwa jumuiya hiyo.
Hatua hiyo inatokana na Serikali hizo kufanya vikao vitatu mfululizo na kuzitenga nchi za Tanzania na Burundi.
Walalamikaji katika kesi hiyo, ni Ally Msangi, David Makata na , John Adam, ambao ni Watanzania, wanaotetewa na wakili Mwandamizi, Jimm Obedi wa jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine, walalamikaji wamewaomba majaji katika mahakama hiyo, kutoa tamko la kusitisha utekelezaji wa maazimio yote ya vikao vya wakuu wa nchi hizo tatu.
Pia wameomba majaji watoe tamko la kukomesha kurejewa kwa vikao kama hivyo kinyume cha mkataba wa jumuiya hiyo.
Kesi hiyo ya aina yake, ilifunguliwa
jana katika Mahakama ya Afrika ya Mashariki na kupokewa na Ofisa
Masijala i katika mahakama hiyo, Boniface Ogoti.
Kufunguliwa kwa kesi hiyo, kunakuja
siku kadhaa baada ya Rais Jakaya Kikwete kuzilalamikia nchi hizo, kuhusu
kuitenga Tanzania kwa kufanya mikutano mbalimbali ya maendeleo ya nchi
zao. Nchi nyingine iliyotengwa ni Burundi.
Kikao cha kwanza cha pamoja
kilifanyika Aprili mjini Arusha kabla viongozi hao kukutana Juni 25 na
26 jijini Entebbe nchini Uganda, walidai kuwa na nia moja ya kurahisha
mawasiliano katika nchi hizo.
Mkutano mwilingine ulifanyika mjini
Kigali Rwanda Oktoba 28 ukiwajumuisha Rais Yoweri Museven wa Uganda,
Uhuru Kenyatta (Kenya), Salva Kiir (Sudan Kusini) na Paul Kagame.
Wakili wa walalamikaji Obedi, alisema
katika kesi ya msingi, wanawashtaki Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya
Rwanda, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Uganda,Mwanasheria Mkuu wa
Serikali ya Kenya na Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo.








.jpg)


Vijana
wa Halaiki wakitoa burudani kwa kuimba nyimbo mbalimbali
zinazohamasisha umoja wa taifa leo wakati wa kilele cha mbio za mwenge
wa uhuru katika viwanja vya Samora mjini Iringa.
Wakimbiza Mwenge wa Uhuru 2013 wakiingia katika viwanja vya CCM Samora mkoani Iringa leo.
Kiongozi wa mbi za Mwenge wa Uhuru 2013 Bw. Juma Ali Simai akisoma
risala ya ujumbe wa wananchi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mh. Jakaya Kikwete leo mjini Iringa.
Rais Jakaya Kikwete (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wakimbiza mwenge wa Uhuru 2013 leo mjini Iringa.
Rais Jakaya Kikwete na mama Salma Kikwete (wa tatu kutoka kushoto)
wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wizara ya Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo wakiongozwa na Waziri wa Wizara hiyo Dkt. Fenella
Mukangara (wa nne kutoka kushoto)
Wananchi
wa mkoa wa Iringa na vijana wa halaiki wakifuatilia matukio mbalimbali
wakati wa Kilele cha mbio za Mwenge leo mkoani Iringa.















Akina mama na watoto wakisubiri kujiorodhesha.


