Friday, September 20, 2013

SITTA AWATETEA WAHAMAJI HARAMU...!!!


Ataka operesheni ifanywe kibinaadamu

• Ahoji kama Watanzania nao watafukuzwa itakuaje

Na Fatuma Kitima,DSM

WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta, ametoa wito kwa mamlaka zinazohusika katika operesheni ya kuwasaka wahamiaji haramu kutumia ubinadamu zaidi katika utelezaji wa zoezi hilo.

Hayo yalisemwa jana wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Sitta alikiri kuna mapungufu katika zoezi hilo na kusema amri ya rais inatakiwa kutekelezwa lakini kwa kuzingatia haki za binaadamu.
Alisisitiza kuwa ubinadamu utumike kwa kuwa baadhi ya wahamiaji hao, wana familia na wamewekeza nchini kwa muda mrefu.

“Baadhi yao wana familia, mali zao sasa endapo atachukuliwa tu ataenda wapi,” alihoji.
Alisema suala hilo linahitaji kufikiriwa kwa kina na kuhoji jee itakuwa vizuri kama Watanzania wanaoishi mipakani mwa nchi jirani nao watafukuzwa.

Kuhusu Tanzania kutoshirikishwa katika mikutano ya wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Sitta alisema nchi hizo zina haki ya kufanya mikutano na kushirikiana katika baadhi ya mambo kwa mujibu wa mkataba iwapo nchi moja itakuwa haijawa tayari kushiriki lakini akasema wanachoomba ni ushirikishwaji.

Alisema kwa sasa Tanzania haijakubaliana na nchi nyengine wanachama wa Afrika Mashariki kuwa ifikapo Oktoba 15 rasimu ya shirikisho iwe tayari jambo ambalo haliwezekani kwa haraka kwakuwa bado kuna mambo matatu hayajatelezeka katika makubaliano.

Aliyataja mambo hayo ni makubaliano ya ushuru wa pamoja, soko la pamoja na mfumo wa sarafu moja.

No comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...